PATA HABARI/MAKALA ZA UHAKIKA

+255-767-402-396

WAZIRI WA JPM AGUSWA NA MIKAKATI WA TAG KWA TAIFA


·      Ni katika  kwa watoto na vijana  hapa nchini
·      Ni wakati wa mapambano ya Haleluya na Yanga
·      Askofu Dk. Mtokambali azitabiria makuu timu  za Tanzania
Mkakati wa uinjilisti ulioasisiwa na kanisa la Tanzania Assemblies of God kupitia Idara zake za Christian Ambassadors  Student Fellowship Tanzania(CASFETA) , Idara ya watoto na Vijana, umemgusa Waziri wa Serikali ya Magufuli na kuipongeza.
Akiongea wakati wa Mchezo uliohusisha Timu za mpira wa miguu Haleluya kuotoa Korea na   Yanga Junior, ya hapa nchini, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na michezo Dk. Harson Mwakyembe alisema kanisa limefanya jambo linaloipa sifa nchi hii kwa mataifa mengine.
Dk. Mwakyembe akihutubia wakati wa mchezo huo uliofanyika katika uwanja wa mpira wa mguu wa Uhuru jijini Dar es Salaam, alisema serikali inaishukuru kanisa la TAG kwa juhudi zake
Dk. Barnabas Mtokambali Askofu mkuu wa kanisa la TAG(kushoto), Waziri wa Habari , Utamaduni, Sanaa na michezo Dk. Harson Mwakyembe na Balozi wa Korea Mh. Song wakati wa pamabano kati wa Haleluya wa Korea na Yanga ya Dar es Salaam.
katika kuwekeza maadili mema na vipaji bora kwa watoto na vijana.
Aidha alisema kuwa ujio wa timu hiyo ya Haleluya iliyokuja hapa nchini chini ya Mwamvuli wa kanisa la TAG ni umetangaza baraka kwa taifa la Tanzania.
Aidha Waziri huyo alisema kufika kwa timu hiyo nchini, haikuwa tu kuitangaza soka la Tanzania kimataifa, bali pia ni kuimarisha urafiki kati ya Tanzania na Korea uliodumu kwa zaidi ya miaka 25.
Tuanatoa shukurani kwa Kanisa la TAG chini ya   Askofu  Dk. Barnabas Mtokambali, kwa kuwezesha timu hiyo ya korea kuja hapa nchini na kufanikiwa kucheza na Yanga Junior,” alisema Dk. Mwakyembe na kuongeza:
“Tunaimani kuwa kupitia mchezo huu umoja na mshikamano kati ya Tanzania na Jamhuri ya Korea utaendelea kudumu na kuwa na tija kwa mataifa mawili.”
Hata hivyo waziri huyo alitoa wito kwa Watanzania wengine kuiga mfano wa kanisa la TAG katika kuzingatia mambo ya msingi yanayotangaza taifa kwa mataifa mengine duniani.
Kwa upande wake Askofu Mkuu wa Kanisa la TAG, Dk. Baranabas Mtokambali aliyekuwa mgeni rasmi wakati wa mechi hiyo alisema mkakati wa mchezo huo ni kuileta Tanzania kwenye Kombe la dunia.
Dk. Mtokambali alisema, kanisa la TAG limeamua kuunga mkakati huo kwa vitendo zaidi kwa kuileta timu ya Haleluya ya korea kucheza na timu ya Yanga ya Tanzania.
Aida Kiongozi huyo wa kiroho alisema kuwa, pamoja na mchezo huo lakini pia kanisa linatumia furasa hiyo kufanya uinjilisti ili kuwaleta watu kwa Yesu.
Tutacheza mchezo lakini pia tutahubiri na injili, hii siyo burudani, au mazoezi ya kujenga mwili kiafya, au kujenga ushirikiano tu, ni njia mojawapo ya kuinjilisha,” alisema Dk. Mtokambali.
Dk. Mtokambali alitumia fursa hiyo kuitabiria mambo makubwa timu za hapa nchini akisema kuwa kwa michezo hiyo itaanza harakati zake za kuifikia kombe la dunia.
Sanjari na mchezo huo wa kirafiki ambao timu hizo zilitoka sare ya bila kufungana, lakini pia uongozi wa kanisa la TAG na ushirika wa Korea ulikabidhi jezi pamoja na mipira ya miguu kwa Waziri huyo kwa ajili ya timu hiyo.
Kanisa lilitumia furasa hiyo kuhubiri mara baada ya mchezo huo kumalizika na kuafanikiwa kuongoza sala ya toba kwa watoto na watu waliohudhuria kutazama mpirab huo.
Aliyehubiri injili ya dakika 15 mara baada ya mechi kumalizika alikuwa na Mkurugenzi mkuu wa Watoto wa kanisa la TAG, Mchungaji Godwin Mjaki.
Mchungaji Mjaki alisema kuwa Mungu ameandaa mpango mzuri kwa ajili ya watoto na kwamba anawahitaji waishi maisha ya kumtegemea yeye.
Mchezo huo wa mpira kati ya Yanga na Haleluya sport club ya Korea, iliandaliwa na kanisa la TAG mahususi kwa ajili ya kupenyeza injili na karama kwa watoto.
Mechi hiyo ilihudhuriwa na watoto zaidi ya 13,000  kutoka katika makanisa ya TAG jijini Dar es Salaam, huku wengine ni ni kutoka shule mbalimbali za msingi hapa jijini.

Mchezo huo pia ulihudhuriwa  na baadhi ya maaskofu wa kanisa la TAG, na makanisa mengine Wachungaji na wakurugenzi wa Idara wakiongozwa na Mkurugenzi wa CASFETA Mchungaji Huruma Nkone ambaye ndiye alikuwa mratibu mkuu.
Share on Google Plus

About Unknown

0 comments: